THRDC yafanya ziara katika Gereza la vijana Wami lililopo mkoani Morogoro Dumila kukabidhi Magodoro Takribani 30 na vifaa vya michezo

Juni 23 2024. Mtandao wa watetezi wa haki za binadamu  - THRDC  umeweza kufanya ziara  katika Gereza la vijana Wami lililopo mkoani Morogoro Dumila kukabidhi Magodoro Takribani 30 na vifaa vya michezo kwa ajili ya vijana katika gereza hilo.

Gereza hilo limeanziahwa mwaka 1968 kama taasisi ya uboreshaji vijana ambalyo ni  taasisi  Pekee na kituo kinachotoa mafunzo  ya fani zaidi ya 7  ikiwemo  fani ya Umeme, Useremala, Uashi/Ujenzi, ushonaji, ufundi bomba,  uchomeleaji na ufundi makenika kwa vijana waliokinzana na sheria.

Akizungumza na  kamishima msaidizi  wa magereza Abdala Hassan Missana ambae ni mkuu wa taasisi hiyo, Mratibu wa Mtandao wakili Onesmo Olengurumwa alisema kuwa ziara hii ni imelenga kukabidhi vifaa hivi kwa vijana  Hawa wafungwa kama moja ya  jitihada za kujakikisha hata wafungwa wanapokuwa katika magereza wanapat haki zao za msingi za binadamu na kukidhi mahitaji yao ya msingi.

Akisisitiza juu haki za binadamu kwa wafungwa magerezani , wakili Olengurumwa alisema ni jukumu la serikali kuboresha miundombinu katika Magereza haya na wadau mbalimbali kusaidia  upatikanaji wa mahitaji   Ya kijamii ili  kulinda ma kudumisha haki za binadamu kwa wote na maeneo yote.

THRDC
24 June 2024